• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

MTWARA YAWEKA MIKAKATI KUKABILIANA NA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KWA WATOTO WA KIKE WENYE UMRI KUANZIA 9 - 14 KUPEWA CHANJO

Posted on: April 19th, 2024

UFUNGUZI WA KIKAO CHA KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) MKOA CHA KUJADILI ZOEZI LA KITAIFA LA UTOAJI WA DOZI MOJA YA CHANJO YA KUZUIA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI (HPV) KWA WASICHANA WENYE UMRI WA MIAKA 9-14

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bi Mwanahamis Munkunda mapema leo hii ameongoza kikao cha ufunguzi cha kamati ya Afya ya Msingi (PHC) Mkoa ambapo ameanza kwa kusema, nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kutuleta pamoja katika kikao hiki. Pili, napenda kuwakaribisha wajumbe wote katika kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ya Mkoa (PHC) kilichoandaliwa rasmi kupeana taarifa na kujadili mikakati ya utakelezaji wa zoezi la kitaifa la utoaji wa dozi moja ya chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 9-14 litakalofanyika nchi nzima kuanzia tarehe 22 hadi 26 Aprili, 2024.

Bi Munkunda akaendelea kusema, ni dhahiri kwamba chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi ijulikanayo kitaalamu kama “Human Papilloma Virus-HPV” ndio mkakati muafaka katika kutokomeza maradhi na kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na saratani ya mlango wa kizazi, hivyo kupunguza gharama kubwa za matibabu kwa familia zetu na Taifa kwa ujumla.

Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) hupendekeza chanjo ya HPV kutolewa kwa wasichana wenye umri wa miaka 9-14. Aidha, hapo awali Tanzania kupitia Wizara ya Afya ilichagua kutoa dozi mbili za chanjo ya HPV kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 pekee. Chanjo hii imekuwa ikitolewa tangu mwaka 2018 na zoezi hili limekuwa likifanywa na Halmashauri zetu kwa kushirikiana na Mkoa, OR-TAMISEMI, Wizara ya Afya na wadau mbalimbali kupitia vituo vya kutolea huduma za afya.

Kaimu Mkuu wa Mkoa akaendelea kusema, Nimefahamishwa kwamba zoezi lenye kuleta mabadiliko ya kutoa dozi moja ya chanjo ya HPV kwa wasichana wenye umri wa miaka 9-14 litafanyika nchini kuanzia tarehe 22 hadi 26 Aprili 2024. Kupitia zoezi hili, Mkoa wetu unatakiwa kuwafikia wasichana wapatao 119,796. Uzoefu wa mazoezi yaliyotangulia unaonesha kwamba mara zote tumevuka malengo tuliyojiwekea kwani idadi hii ni makisio tu na siyo idadi kamili ya walengwa wote waliopo kwenye jamii.

Munkunda akasisitiza kuwa, zoezi hii litafanyika kupitia shule za msingi na sekondari kwani walengwa wengi hupatikana shuleni, na kupitia vituo maalumu vilivyoandaliwa mitaani kwa ajili ya wasichana waliopo nje ya mfumo wa shule.

Akamalizia kwa kutoa wito kwa viongozi wote katika Mkoa, kuhakikisha wanapeleka ujumbe kwa jamii kuhusu kufanyika kwa zoezi hili ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha na kuwaelekeza wananchi kutoa ushirikiano kwa wataalamu wanaotekeleza zoezi hili muhimu. Chanjo hizi ni salama, hazina madhara yoyote, zimethibitishwa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA).

Aprili 19, 2024

Wizara ya Afya Tanzania

World Health Organization (WHO)

#TunaifunguaMtwara

#KaziIendelee

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.