• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Ndovu Resources watumia milioni 720 kusukuma maendeleo Mtwara

Posted on: April 5th, 2017

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda (mwenye suti nyeusi) akipokea msaada wa vitabu toka kwa Mwakilishi wa kampuni ya Ndovu Resources LTD, James Chialo. Anayefuata kutoka kushoto ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Kanuda Nswira. Kaimu Mkurugenzi Mkurugenzi Manispaa ya Mtwara Mikindani, Sambwe Sijabaje. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya Mtwara, George Mrisho. (Picha na Jamad Omari, Afisa Habari Manispaa ya Mtwara Mikindani)


Kampuni ya Ndovu Resources LTD inayoshughulika na utafiti wa mafuta na gesi asilia mkoani Mtwara imetumia shilingi milioni 720 kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo mkoani hapa. Misaada hiyo imekuwa ikitolewa katika sekta za afya, elimu, maji na miundombinu ya ujenzi.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda Wakati akipokea msaada wa vifaa tiba kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Ligula pamoja na vitabu kwa ajili ya shule za mkoani Mtwara vilivyotolewa na kampuni hiyo.

Ametaja baadhi ya misaada ambayo kampuni hiyo imekuwa ikitoa kwa nyakati tofauti kuwa ni pamoja na gari la kisasa la kubebea wagonjwa, vitanda vya wagonjwa, vifaa tiba. Pia msaada wa saruji kwa ajili ya ujenzi wa kondo, vyote vikiwa vimetolewa kwa nyakati tofauti katika hospitali ya Nanguruwe iliyoko wilayani Mtwara.

Kwa upande wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Ligula mapema mwaka jana kampuni hiyo ilitoa msaada wa vitanda vya kisasa pamoja na vifaa tiba.

Aidha, Ndovu Resources wameweza kusaidia vitanda na magodoro ya wagonjwa kwa zahanati za Nkunwa, Chawi na Mbawala zilizoko mkoani Mtwara.

Mheshimiwa Mmanda ameshukuru na kuwapongeza Ndovu Resources kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakijitolea kusaidia maendeleo na kutatua changamoto nyingi za mkoa wa Mtwara.

Akikabidhi msaada wa vifaa tiba na vitabu vya ziada kwa kaimu Mkuu wa Mkoa, mwakilishi wa kampuni hiyo, James Chialo amesema Ndovu wana wajibu wa kusaidia jamii katika maeneo wanayofanya kazi hivyo wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha jamii inanufaika na uwekezaji wao. Licha ya msaa huo, wako katika mchakato wa kutoa huduma ya maji kwa vijiji vya Namayakati shuleni na Namayakati barabarani vilivyoko Wilayani Mtwara.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanuda Nswila amewashukuru Ndovu Resource na kuwataka wadau wengine kuiga mfano wao kwa kujari jamii inayowazunguka. Aidha amewataka Ndovu Resources LTD kuwa na utamaduni wa kuweka nembo ya kutambulisha misaada yao mingi ambayo wamekuwa wakitoa ili iwe alama ya utambulisho kwa mazuri wanayoyafanya.

Kampuni ya Ndovu ilipata leseni ya kufanya utafiti katika mikoa ya Lindi na Mtwara mwaka 1999. Hadi sasa wameshafanya utaafiti na uchimbaji katika maeneo ya Songosongo na Nyuni mkoani Lindi, pia Likonde,  Ntorya1 na Ntolya 2 katika mkoa wa Mtwara.


kutazama video ya tukio zima bonyeza HAPA


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.