• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

NIDA kutoa vitambulisho vya Taifa Mtwara

Posted on: November 8th, 2017

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Rose Joseph aakizungumza na viongozi wa Mkoa wa Mtwara wakati wa uzinduzi wa uandikishaji wa utoaji wa vitambulisho vya Taifa kwa wakazi wa mkoa wa Mtwara


Wakazi wa mkoa wa wa Mtwara wanatarajia kunufaika na mpango wa utoaji wa vitambulisho vya taifa unaosimamiwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA). Mpango huu unaotarajiwa kuanza Novemba 13, mwaka huu unakusudia kuwafikia wakazi zaidi ya 1,121,663 walioko mkoani hapa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo uliofanyika katika ukumbi wa Boma Mkoa ulioko Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara jana, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Rose Joseph amesema zoezi hili litaanza Novemba, 13 mwezi huu na kwamba kufikia Februali 2018 wanatarajia kuwa wamekamilisha kuandikisha wananchi wote na hatimaye kutoa namba za vitambulishio wakati vitambulisho vikiendelea kuzalishwa.

Anasema zoezi hili linakuja kwa mara ya pili baada ya kukamilika kwa zoezi la awali lililowahusisha watumishi wa Umma lililofanyika mapema mwaka huu. Aidha mwaka 2014 kulifanyika zoezi la kuandikisha wananchi ambapo hatua za ujazaji wa fomu ulifanyika.

Amewataka wale waliojiandikisha mwaka 2014 katika zoezi lililofanyika nchi nzima kujitokeza katika vituo vya kuandikisha ili kupata maelekezo yatakayowezesha taaifa zao kuingizwa katika mfumo wa sasa wa kielektloniki.

Kwa upande wake Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda aliyekuwa akimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Gelasius Byakanwa amewataka wananchi wa kuchangamkia fursa hiyo kwani ni muhimu kwa maendeleo yao.

Amesema kitambulisho cha Taifa kitawawezesha wananchi kupata fursa mbalimbali kama vile ajira, nafasi za uongozi, Afya, uchumi na mengine mengi.

Amewataka wakuu wa wilaya wote, wakurugenzi, Makatibu Tawala wa Wilaya, Viongozi wa Dini, wahakikishe wanasimamia zoezi hili kwa weledi ili kuhakikisha linafanikiwa.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda amewataka wakurugenzi na viongozi wote wa Mkoa kutoa ushirikiano ili kuepusha kasoro zitakazoweza kujitokeza. Amesema kwa jiografia ya mkoa wa Mtwara ulioko mpakani, kuna uwezeakano wa raia wa kigeni kujipenyeza ili kupata vitambulisho hivyo. Amewataka watu wote kuwa makini ili kuhakikisha kasoro hizo hazijitokezi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2022 November 24, 2021
  • Majina ya watumishi wa umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo February 09, 2018
  • KUFANYA MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19 August 30, 2021
  • Matokeo ya Kidato cha NNe 2017 January 30, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MKUU WA MKOA KUTILIA MKAZO ELIMU NA UKUSANYAJI MAPATO

    August 04, 2022
  • Zingatieni Sheria ya Mazingira. ‘’Jafo’’

    December 20, 2021
  • BILIONI 268 KUMALIZIA BARABARA YA MTWARA – NEWALA HADI MASASI KWA KIWANGO CHA LAMI

    November 25, 2021
  • BANDARI YA MTWARA KUPOKEA MELI KUBWA NA KUSAFIRISHA MAKAA YA MAWE KWENDA NJE YA NCHI.

    November 01, 2021
  • Tazama Zote

Video

Wakulima Mtwara wachangamkia kilimo cha Ufuta
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • NBS
  • IKULU
  • UTUMISHI
  • SALARY SLIP
  • e-GA

Kurasa Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.