• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

PAZENI SAUTI; KATAENI UKATILI WA KIJINSIA_RC KANALI AHMED ABBAS AHMED.

Posted on: December 10th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameitaka jamii kutofumbia macho watu wanaotekeleza ukatili wa kijinsia kwani kwa kufanya hivo ni kuchochea ongezeko la vitendo hivyo.


Kanali Abbas ametoa kauli hiyo leo katika maadhimisho ya  siku 16 za kupinga  ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Nanyamba Ufundi katika halmashauri ya Mji wa Nanyamba ambapo aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Dunstan Kyobya.


Katika hotuba yake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Abbas amesema ongezeko la vitendo vya ukatili wa kijinsia ni jambo ambalo halikubaliki na hivo kuwataka wananchi katika ngazi zote kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi wanapowabaini wahusika.


Aidha katika hotuba hiyo ya  Mkuu wa Mkoa  iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Dunstan Kyobya iliongeza kuwa jitihada za serikali za kupambana na vitendo hivyo viovu zitafanikiwa endapo mapambano yataanzia katika ngazi ya familia, watu binafsi, shuleni, maofisini, katika nyumba za ibada, na pia katika majukwaa ya michezo.


Katika hotuba hiyo Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameonyesha kusikitishwa na ongezeko la vitendo vya ukatili kijinsia ambapo kuanzia Januari mpaka sasa takwimu zinaonyesha jumla ya watu 223  wamefanyiwa ukatili wa kijinsia mkoani Mtwara, huku akiitaka jamii kupaza sauti juu ya wanaotekeleza vitendo hivyo kwa kutoa taarifa kwa vyombo vinavyotoa msaada wa kisheria.


Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Nanyamba Ufundi yakiwa na kauli mbiu "Kila uhai una thamani tokomeza mauaji na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto" ambayo yalihudhuriwa na mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali pamoja na wakuu wa wilaya 5 za Mkoa wa Mtwara.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.