• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC Byakanwa afanya ziara ya kushtukiza shuleni. Abaini mapungufu ya usimamizi wa shule kwa Walimu Wakuu.

Posted on: January 23rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa akisaini Kitabu cha Wageni katika Shule ya Msingi Maendeleo


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Gasper Byakanwa amefanya ziara ya kushtukiza kwenye shule za msingi na sekondari Manispaa ya Mtwara Mikindani na kubaini mapungufu ya  usimamizi wa shule hizo toka kwa wakuu wa shule.

Shule alizotembelea ni shule ya Sekondari Rahaleo, pamoja na shule Nne za Msingi ambazo  ni Shule ya Msingi Maendeleo, Raha Leo, Lilungu na Shule ya Msingi Mivinjeni.

Akiwa ameambatana na Kaimu Afisa Elimu Mkoa, Sallum Masalanga Mheshimiwa Byakanwa amebaini mapungufu ya usimamizi wa Walimu Wakuu wa shule hizo ambayo ni pamoja na Wakuu hao kutokuwa na taarifa za walimu ambao hawapo katika eneo la kazi kwa sababu mbalimbali wakiwemo wenye likizo za ujauzito. Pia walimu kutofuata taratibu za kiutumishi wanapoomba ruhusa ya kwenda nje ya kituo cha kazi.

Mapungufu mengine ni walimu wakuu kutopanga mikakati na walimu wao juu ya kuongeza ufaulu jambo aliloliagiza katika kikao na wadau wa elimu kilichofanyika mwanzoni mwa mwezi huu. Aidha walimu hao wameshindwa kutimiza agizo alilolitoa kwenye kikao cha wadau wa elimu ambapo aliagiza kubandikwa majina ya wanafunzi walio faulu mitihani ya taifa mwaka 2017 na walimu waliowezesha wanafunzi hao kufaulu.

Kufuatia hali hiyo Mheshimiwa Byakanwa amemuagiza Kaimu Afisa Elimu Mkoa Salum Masalanga ampatie maelezo juu ya walimu ambao hakuwakuta kazini.

Huu ni mwendelezo wa utaratibu aliojiwekea Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kuhakikisha ufauru kwa wanafunzi mkoani Mtwara unabadilika.

Katika matokeo ya kidato cha pili yaliyotangazwa hivi karibuni mkoa wa Mtwara ulishika nafasi ya 26 kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara.


Kufuatia matokeo hayo yasiyorodhisha Mheshimwia Mkuu wa Mkoa alifanya kikao na wadau wa elimu na kupeana mikakati ya kuhakikisha hali ya ufaulu inabadilika ambapo wadau hao waliwekeana mikakati ambayo anafuatilia utekelezaji wake..





Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.