Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe.Kanali Patrick Sawala amewataka viongozi wa vyama vya ushirika kutatua changamoto za wakulima zilizojitokeza wakati msimu wa korosho wa mwaka 2024 .
Mhe. Sawala amezieleza baadhi ya changamoto zilizokuwepo msimu uliopita leo 24 juni, 2025 kuwa ni pamoja na wakulima kutolipwa kwa wakati na kulipwa malipo tofauti na stahiki zao.
“Ndugu zangu fuatilieni malipo ya wakulima wapate fedha zao kwa wakati, pia niwaombe Bodi ya korosho na vyama vya ushirika msimu huu muanze maandalizi mapema ili kuepuka changamoto kwa wakulima kutolipwa kwa wakati” amesema kanali Sawala.
Kwa niaba ya vyama vikuu vya ushirika mkoani Mtwara Bw. Karimu Chipola Mwenyekiti wa TANECU amesema “Soko la awali ndio changamoto kubwa yaani viongozi wa vyama wanauza korosho bila kuwashirikisha wakulima hivyo inapelekea wakulima kulipwa fedha nusu ya matarajio yao”
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara
Anuani ya Posta: 544, MTWARA
Simu: +255 23 2333014
Mobile: +255 23 2333014
Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz
Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.