• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

Posted on: June 21st, 2025

Mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala amewataka viongozi wa vyama vya msingi na wanachama wa vyama vya msingi mkoani Mtwara kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wabadilike na kufanya kazi kwa uadilifu ili kuleta tija kwa wakulima.

Kanali Sawala ametoa agizo hilo wakati anazungumza na viongozi hao kwenye jukwaa la ushirika lililokuwa na lengo la kujadili changamoto na mafanikio katika sekta ya ushirika mkoani humo.

Amesema wale viongozi wa ushirika wanaofanya ubadhirifu wa fedha za wakulima kwa makusudi ili kujinufaisha waache mara moja kufanya hivyo wakiendelea mkono wa sheria utawashughulikia.

Kanali Sawala amewasisitiza viongozi hao kuacha kuchukua fedha za wakulima ambapo tumeanza msimu wa ufuta kisha mbaazi zitafuata sitaki kusikia mkulima amedhulumiwa hela zake naaamini hata msimu wa korosho ukifika fanyeni vizuri sitaki kusikia malalamiko ya wakulima.

Mkuu huyo wa mkoa ametumia jukwaa hilo kuwataka viongozi hao kujipanga kuongeza uzalishaji katika mazao yote ikiwemo korosho, ufuta, mbaazi na sasa ni zao la choroko lakini pia wakumbusheni wakulima kulima mazao mchanganyiko yakiwemo mazao ya chakula na biashara ili kujiongezea kipato.

Halikadhalika Kanali Patrick Sawala amezitaka taasisi za kifedha mabenki kufanya taratibu zao kwa umakini ili waweze kulipa fedha za wakulima kwa wakati bila mkulima kupata usumbufu wa kucheleweshewa malipo yake.

Katika hatua nyingine amewasisitiza viongozi wa vyama vikuu vya ushirika ambao ndio wasimamizi wakuu wa ushirika kusimamia ipasavyo malipo ya wakulima katika msimu huu yaende vizuri na katika misimu yote inayokuja malipo yaende vizuri kwa wakulima sambamba na kuwataka waendesha maghala ambao sio waaminifu wamekuwa wakileta changamoto kwenye kuhifadhi mazao wasipewe nafasi ya kupewa maghala.

Akihitimisha hotuba yake kwenye jukwaa hilo la ushirika mkuu wa mkoa wa Mtwara kanali Patrick Sawala amewakumbusha viongozi kuhakikisha wanapiga kura kwenye uchaguzi mkuu ifikapo Oktoba mwaka huu kwa amani na utulivu .


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.