• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC SAWALA AZIAGIZA TAASISI KUANZISHA MABARAZA YATAKAYOSHUGHULIKIA KERO ZA WAFANYAKAZI

Posted on: May 1st, 2025


Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Sawala amewataka wafanyakazi kufanya kazi bila kubagua huku akiwataka kutoa huduma nzuri kwa wananchi wanaowahudumia. Amezungumza hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya wafanyakazi Duniani yaliyofanyika mapema leo tarehe 01 Mei 2025 katika viwanja vya Sabasaba wilayani Newala.

Kanali Sawala pia amewataka waajiri na wafanyakazi kushirikiana huku akiwataka waajiri kutoa mikataba inayofuata sheria ili wasiwe na migogoro katika sehemu zao za kazi na kuleta maendeleo.

“Naagiza kila Taasisi kuanzisha mabaraza ya wafanyakazi ambayo yatajadili na kushughulikia changamoto za watumishi kazini.” amesema Kanali Sawala.

Katika hatua nyingine, Kanali Sawala ametoa rai kwa wafanyakazi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 huku akiwasisitiza kuchagua viongozi bora.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, CPA. Bahati Geuzye, ametoa wito kwa wafanyakazi kuipenda Mtwara na kuacha tabia ya kutafuta uhamisho kila mara huku akisisitiza kuwa kuhama sio suluhisho la kila changamoto.

Maadhimisho hayo yameambatana na ugawaji wa vyeti na zawadi Kwa wafanyakazi bora wa mwaka katika kila idara kutoka Halmashari na wilaya zote za Mkoa wa Mtwara.

Kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika mkoa wa Singida yakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo ametangaza kuwa Serikali itaongeza kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma kwa 35% kutoka Shilingi 370,000/= hadi kufikia 500,000/= kuanzia mwezi Julai 2025.

Kauli mbiu iliyobeba maadhimisho hayo ni “Uchaguzi Mkuu 2025 utuletee Viongozi wanaojali hali na maslahi ya wafanyakazi, Sote tushiriki.”

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.