• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

SEKTA YA VIWANDA ZINGATIENI SHERIA- WAZIRI WA BIASHARA, VIWANDA NA UWEKEZAJI_DKT: ASHATU KIJAJI

Posted on: January 7th, 2023

Waziri wa Biashara, Viwanda na uwekezaji Mhe. Dkt Ashatu Kijaji amefanya ziara ya siku moja ndani ya mkoa wa Mtwara siku ya tarehe 07 Januari, akiambatana naibu waziri wa madini Mhe. Dkt Steven  Kiruswa lengo likiwa ni kukakugua maeneo yote ya uwekezaji na kutatua migogoro.

 Halikadhalika katika ziara hiyo Dkt. Kijaji ametembelea kiwanda cha sukari cha S.J sugar pamoja na kiwanda cha chumvi na baadhi mashamba ya chumvi kisha kupata nafasi yakuongea na wazalishaji wa chumvi na kusikiliza kero zao.

Akitoa maelekezo ya Serikali baada ya kukagua eneo la kiwanda cha sukari katika Kata ya Kitele, Halmashauri ya wilaya ya  Mtwara,  Dkt.  kijaji ametoa miezi 3 ya utekelezaji kwa  muwekezaji wa kiwanda hicho.

"Sasa tumepita hapa kwenye alichokiita yeye ni kitalu kwa ajili ya mbegu ili ahamishie kwenda kwenye shamba lake kubwa la miwa, tunaona hapa hakuna kitalu cha mbegu ya miwa ila kuna miwa iliyokauka, kwahiyo huyu bwana ameidanganya Serikali, ninampa miezi mitatu, aanzishe vitalu vingine kwa ajili ya mbegu ili aweze kulitumia vizuri eneo la ekari 4100 alilopewa” alisema Dkt. Kijaji.

Aidha amemtaka muwekezaji wa S.J sugar kufanya uwekezaji katika kilimo cha miwa kama alivyosema katika mkataba wake kwani lengo la serikali ni kwamba, mpaka kufikia Disemba 2023 taifa letu lisiwe na upungufu wa sukari.

Pia Mhe. Dkt Kijaji ametoa maelekezo ya Serikali kwa wakulima wa chumvi na kuwataka wawe watulivu kwani Serikali inatambua uhaba wa soko la chumvi na wawekezaji nchini na serikali iko tayari kuwasaidia. Amewataka wakulima wa chumvi kuweka takwimu vizuri za uzalishaji wao kwa mwaka ili serikali ijue ni namna gani ya kuwashawishi wawekezaji kuwekeza katika uchakataji wa chumvi ghafi.

"Ndani ya taifa letu hatuna upungufu wa chumvi ghafi, kwa maana hiyo hatuna sababu ya msingi ya kuendelea  kuruhusu chumvi ghafi iletwe kutoka nje ya nchi kuja ndani ya taifa letu, tulilifanyia kazi jambo hili kwa mda mrefu ,tumekaa na kama serikali tumekubaliana  sasa ni mwisho kwa wale wanaoleta chumvi ghafi kutoka nje, kama analeta chumvi ghafi kutoka nje, awe ameshanunua yote tuliyonayo hapa ndani kwanza" alisema Dkt. Kijaji.

Vilevile ameongeza kuwa Mhe rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameamua kuilea sekta binafsi na hivo yuko tayari kuwasaidia na tarehe 11 Januari kutakuwa na mkutano mkubwa wa kikodi utakaoshirikisha wadau wote wa uwekezaji na viongozi wa serikali.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU 2025 KUPOKELEWA MKOANI MTWARA MEI 17

    May 15, 2025
  • MTWARA TUKO TAYARI KUUPOKEA NA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025

    May 14, 2025
  • UFUTA NA MBAAZI KUPIMWA KIDIGITALI MKULIMA KUPATA RISTI KUPITIA SIMU YAKE

    May 14, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE. KANALI PATRICK SAWA AKAGUA MRADI WA MAENDELEO TANDAHIMBA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.