• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

SERIKALI IMEWEKA REKODI BILIONI 619.6 KUINUFAISHA MTWARA - KANALI AHEMD ABBAS AHMED _ MKUU WA MKOA WA MTWARA

Posted on: July 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita imeweka historia Mkoani Mtwara kwa kuwekeza kiasi cha shilingi bilioni 619.6 kutekeleza miradi ya kimkakati.


Kanali Abbas ametoa kauli hiyo wakati akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Taifa Mhe. Daniel Chongolo katika Mkutano wa hadhara katika uwanja wa CCM Nangwanda mjini Mtwara na kusema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo katika sekta za Afya, Elimu, Maji, barabara na umeme umeongeza tija katika shughuli za maendeleo na hivyo kuwapunguzia kero wananchi.


"Mhe Katibu Mkuu nikianza kuelezea mafanikio yaliyotokana  na uongozi bora wa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na CCM nadhani tutakesha, itoshe kusema imeweka rekodi ambayo haitasahaulika kwa Wanamtwara" aliongeza Kanali Abbas.


Pia Kanali Abbas ameishukuru serikali kwa hatua inazochukua kutatua kero za watumishi wa umma hatua ambayo amesema imeongeza hamasa miongoni mwao.


"Mhe Katibu Mkuu katika kipindi Cha miaka miwili tumeshuhidia watumishi 4432 wakipandishwa madaraja na Wakati huo huo serikali ikiajiri watumishi 553 na kuwaleta Mkoani Mtwara" alisisitiza Kanali Abbas.


Aidha Kanali Abbas  amemweleza Katibu Mkuu Chongolo kuwa serikali inayoongozwa na CCM kwa kipindi chote imekuwa mstari wa mbele kutatua kero za wakulima wa Mkoa wa Mtwara hususani wanaolima Korosho na kusema kuwa katika msimu huu tayari pembejeo kiasi Cha Tani 10,737,000 zimepokelewa.


Wakati huo huo Kanali Abbas amelitumia jukwaa la Mkutano huo kumweleza Katibu Mkuu kuwa Wanamtwara wanaunga Mkono makubaliano ya Uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam yanayohusisha serikali za Tanzania na Dubai akisisitiza kuwa hatua hiyo itaongeza tija katika utendaji wa sekta ya Bandari nchini ikiwemo Bandari ya Mtwara.


"Kwa upande wetu sisi Wanamtwara tunaamini mkataba huu utakuwa na manufaa makubwa, sambamba na hilo tunaomba kuanzia Sasa Korosho yetu ianze kusafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara" alisisitiza Kanali Abbas.


Mkutano huo wa hadhara umehudhuriwa na baadhi ya Mawaziri, wakuu wa Mikoa ya Lindi na Ruvuma, viongozi mbalimbali wa Chama pamoja na wanachama wa CCM.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.