• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

SERIKALI YATOA BILIONI 8 KUTEKELEZA MIRADI 7 YA MAJI

Posted on: October 24th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema uwekezaji unaofanywa na serikali ya awamu ya sita katika sekta ya maji ni kielelezo cha serikali ya mfano yenye kiu ya kutatua kero za wananchi wake.

Kanali Abbas ametoa kauli hiyo katika hafla ya utiaji saini mikataba 7 ya miradi mikubwa ya maji itakayotekelezwa katika wilaya za Mtwara na Tandahimba kwa gharama ya Zaidi ya shilingi bilioni 8 na kuongeza kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kutaondoa kero ya maji kwa wakazi wa vijiji vitakavyonufaika na hivyo kuwawezesha kutekeleza shughuli zao za kiuchumi bila kikwazo.

“ Ndugu viongozi na wanahabari mliopo hapa kupitia miradi hii iliyotiwa saini hii leo bila shaka sote tunajionea dhamira ya dhati ya serikali ya awamu ya sita ya kumtua mama ndoo kichwani, tumeishuhudia mikataba yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 8 ikisainiwa, cha ajabu utakuta bado kuna baadhi ya watu wanabeza jitihada hizi, jamani hivi hawaoni” alihoji kanali Abbas.

Aidha kanali Abbas pia kupitia jukwaa la hafla hiyo amewaagiza viongozi katika ngazi mbalimbali kuhakikisha wanasimamia kwa karibu miradi hiyo ili iweze kutekelezwa katika viwango vya ubora vinavyoendana na thamani halisi ya fedha iliyotumika.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Kanali Patrick Sawala ambaye Wilaya itanufaika na miradi hiyo amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa atashirikiana kikamilifu na watendaji katika ngazi zote ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa tija huku akiwataka wakandarasi waliopewa kazi hiyo kukamilisha kwa wakati.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bi Mwanahamisi Munkunda amemtaka kila mwananchi inakopita miradi hiyo kuwa balozi kwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan za kutafsiri kwa vitendo dhana ya kumtua mama ndoo.

Meneja wa Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) Primy Damas amesema pindi miradi hiyo itakapokamilika itanufaisha wakazi zaidi ya 67,000 katika vijiji 35 vya Wilaya za Mtwara na Tandahimba.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.