• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

SHIRIKIANENI NA SERIKALI YA MKOA KUONGEZA UFANISI KATIKA MIRADI YA JESHI LA UHAMIAJI – MHE. KASPAR MMYA, KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Posted on: February 14th, 2023

Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya ndani Mhe. Kaspar Mmuya amefanya ziara ya siku moja katika Mkoa wa Mtwara lengo likiwa ni kukagua miradi ya maendeleo ndani ya Jeshi la Uhamiaji. Katika ziara hiyo Katibu Mkuu Mmuya amemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed ambapo wamekubaliana kuimarisha mahusiano kati ya serikali ya mkoa, taasisi linazozisimamia pamoja na wadau wote ili kuongeza tija katika miradi inayotekelezwa Mkoani humo.

Katika kikao cha ndani na Mkuu wa Mkoa na Kamati yake ulinzi na usalama Mhe. Mmuya amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali ya mkoa na taasisi za vyombo vya ulinzi na Usalama hatua ambayo itadumisha mshikamano, umoja na Ari ya kujitoa kudumisha  Amani na Usalama hususani katika maeneo ya mpakani ambapo Tanzania inapakana na nchi jirani.

Aidha Katibu Mkuu Mmuya amewataka viongozi wa majeshi wa mkoa, kushirikisha uongozi wa Mkoa katika miradi yote wanayoitekeleza kwa kutoa taarifa sahihi za uzalishaji na utekelezaji wake ili serikali ya Mkoa na wadau wake waweze kushauri au kupendekeza njia Bora inayoweza kuzinufaisha pande zote mbili hatua ambayo pia itasaidia kuchangia kikamilifu kukuza pato la Mkoa.

“Jukumu la ulinzi na usalama ni la kwetu na siyo tu ndani ya Mkoa bali ni kwa Nchi nzima naamini tutafanikiwa tu endapo tutashirikiana kwa karibu katika hatua zote za utekelezaji wa majukumu tuliyopewa, hivyo nawasihi askari wote kwa nafasi zao wakilinde kiapo chao,  wasilale, kuhakikisha Nchi yetu iko salama” alisema Mhe. Mmuya.

Pia ameuomba uongozi wa mkoa kuridhia ombi la kutenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za uhamiaji katika maeneo yaliyopendekezwa ili kuimarisha ulinzi na Usalama.

“Mpaka sasa tumefanikiwa kutekeleza mradi wenye ofisi nne mpya zilizopo Nanyumbu, Masasi, Newala, na Kilambo ambazo bado hazikidhi mahitaji hasa kwa kanda hii ya kusini ambayo ina changamoto ya kutembelewa na wageni kutoka nchi jirani zinazopakana na Tanzania ikiwemo Msumbiji.

“Mhe. Mkuu wa Mkoa tunashukuru Ofisi zimejengwa lakini hazina nafasi ya kutosha kulingana na Majukumu yetu, hivyo basi nikuombe uzungumze na viongozi wako wa halmashauri muone ni kwa kiasi gani mnaweza kutusaidia kupata eneo kwa ajili ya ofisi kuu” aliongeza Mhe. Mmuya.

Halikadhalika Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amemshukuru Katibu Mkuu kwa uamuzi wake wa kufanya ziara katika Mikoa ya Kusini ambapo amejionea hali halisi ya utekelezaji wa miradi iliyoko chini ya Jeshi la Uhamiaji na kusema kuwa hatua hiyo itaongeza ufanisi na Ari kwa watendaji ndani ya jeshi hilo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.