• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

SIMAMIENI UKUSANYAJI WA MAPATO KUONGEZA KASI YA MAENDELEO: KANALI AHMED ABBAS AHMED.

Posted on: June 2nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amevitaka vyama vya Ushirika  kuweka utaratibu mzuri wa ukusanyaji mapato ili yaweze kuchangia kuongeza kasi ya maendeleo.


Kanali Abbas ameyasema hayo katika mkutano wa jukwaa la maendeleo ya ushirika mkoa wa Mtwara kwa mwaka 2023 uliofanyika katika ukumbi wa Polisi Mess na kusisitiza kuwa vyama hivyo vinapaswa kusimamia sekta ya kilimo kikamilifu ili kuboresha maisha ya wakulima.


“Nyinyi kama vyama vya ushirika msipoweka utaratibu  mathubuti wa kudhibiti suala la ukusanyaji wa mapato  kulingana na matarajio ya mkoa ni dhahiri kwamba sekta ya kilimo na maendeleo ya mkoa yatayumba” alisistiza Kanali Abbas.


Miongoni mwa maagizo ya Mkuu wa Mkoa katika mkutano huo ni pamoja na  viongozi wa vyama vya ushirika kusimamia maadili,  kutembelea wanachama, kuendesha vikao na kuandaa taarifa za mapato na matumizi na mipango ya vyama swala ambalo litachangia kurahishisha utatuzi wa changamoto na kuongeza tija katika utoaji huduma kwa wakulima.


Halikadhalika  Kanali Abbas  amesisitiza juu ya umuhimu wa  matumizi ya matokeo ya tafiti mbalimbali za kilimo zilizofanyika sambamba na matumizi ya Tehama kwa wanachama wa vyama hivyo ili kuongeza uzalishaji wa mazao.


Awali, akimkaribisha Mkuu wa Mkoa katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Hanafi Msabaha amewasihi viongozi  wa vyama vya ushirika  kudumisha umoja miongoni mwao jambo litakaloongeza ufanisi katika sekta ya kilimo kwa ujumla.


Pia amewataka viongozi hao kwenda kusimamia ubora wa mazao yanayokusanywa kutoka kwa  wakulima kama njia ya kuyaongezea thamani katika soko na kuongeza kuwa imebainika kuwa sababu inayochangia kushuka kwa soko la mazao hayo ni udanganyifu unaofanywa na baadhi yao kwa kushirikiana na wakulima wachache wakati wa kupokea mazao kabla ya mnada.


 MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.