• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

TACOBA yachanja mbuga kuuza hisa.

Posted on: August 7th, 2017


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego akimkabidhi Mwakilishi wa ITV Mtwara, Lucy Ogutu vielelzo vyake baada ya kunua hisa katika Benki ya TACOBA


Benki ya wananchi wa Tandahimba (TACOBA) imeendelea na Mikakati yake ya kujiimarisha kwa kuuza hisa zake ikiwa ni lengo la kuongeza mtaji. Akizungumza na wananchi wakati wa zoezi la harambee ya ununuzi wa hisa za Benki hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Tandahimba jana Meneja Mkuu Benki ya TACOBA Mgwagi Stephen amesema mipango yote ya kuifanya Benki hiyo iwe Benki shindani katika huduma za kibenki hapa nchini imekamilika.

Ameitaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuhakikisha Benki inauza hisa zake ndani na nje ya wilaya ya Tandahimba ikiwa ni lengo la kuifanya iwe Benki ya watu wa kusini hapo baadaye.

Katika harambee hiyo iliyofanikisha ahadi ya shilingi milioni 752 amesema zipo changamoto nyingi zilizojitokeza tangu imeanzishwa lakini uzoefu umewaonesha kwamba hakuna lisilowezekana. Amewataka wananchi wote kuchangamukia hisa hizo zinazouzwa shilingi 1000 kila moja.

 Amesema sheria za Tanzania zinataka benki iwe na mtaji unaoanzia bilioni 5 jambo ambalo hawajalifikia. Amesema kwa sasa benki hiyo iliyoanzishwa miaka ya 2000 ina mtaji wa shilingi milioni 999,482. na kwamba mikakati yao ni kufikia malengo katika kipindi kifupi na hatimaye kuwa Benki ya wananchi wote wa ukanda wa Kusini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego aliyeongoza harambee hiyo amesema mambo yote yanawezekana na kwamba katika mazingira ya uchumi wa Wilaya ya Tandahimba inayoongoza kwa kuzalisha korosho hapa nchini, Bilioni 5 ni kidogo endapo kweli wananchi wa Tandahimba wataamua kuwekeza.

Amesema kuwekeza katika Benki kuna faida kubwa ikiwa ni pamoja na kuwa sehemu ya mmiliki wa benki hivyo kushiriki katika faida inayopatikana kutokana na Benki hiyo.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba, Said Msomoka amesema wanatambua umuhimu wa kuwa na Benki hiyo na ndiyo maana halmashauri iliamua kununua hisa na hatimaye kumiliki asilimia 49 ya hisa za Benki hiyo. Vilevile katika bajeti ya mwaka 2017/2018 wametenga shlingi milioni 600 kwa ajili ya ununuzi wa hisa mpya. Msomaoka amewataka wananchi wa Tandahimba kuchangamukia furasa hiyo.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA "ACHENI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"

    June 21, 2025
  • MTWARA MWENYEJI WA MAFUNZO YA KOROSHO BARA LA AFRIKA.

    June 23, 2025
  • NHIF YAFANYA MAZUMGUMZO NA RC SAWALA

    June 23, 2025
  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA

    June 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.