• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

TIMIZENI WAJIBU WENU KATIKA MALEZI YA WATOTO KUJENGA FAMILIA BORA: KANALI AHMED ABBAS AHMED.

Posted on: May 15th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa malezi kwa watoto hatua ambayo amesema itapunguza vitendo vya mmomonyoko wa maadili na hivyo kujenga familia bora zenye upendo zinazotatua matatizo yake kwa njia ya mazungumzo ili kutoa fursa kwa wazazi na watoto kuyapatia ufumbuzi.

Kanali Abbas ameyasema hayo wakati akifungua kongamano la Siku ya kimataifa ya familia lililofanyika katika ukumbi wa Chuo  cha Ualimu Ufundi mjini Mtwara na kusisitiza kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kutambua umuhimu wa familia na mchango wake maendeleo ya jamii na uchumi wa taifa jambo ambalo litapata tija kwa kuwashirikisha wadau kuanzia nagazi ya familia waweze kujadili na kupanga mikakati ya utekelezaji.

Aidha, Kanali Abbas amewakumbusha wazazi kutekeleza msingi wa malezi hasa kwa kujua na kutimiza majukumu yao ya kuwalinda watoto katika maeneo ya msingi ikiwemo kuwatimizia mahitaji yao ya  msingi, kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili sambamba na kuzungumza nao moja kwa moja ili  kutambua changamoto zinazo wakabili na maendeleo yao kwa ujumla.


Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii, Mkoa wa Mtwara Bi  Tabitha kilangi amesema kuwa Maadhimisho ya Siku ya familia duniani yanalenga kuhamasisha, kuhimiza, kuelimisha na kuiamsha  jamii kuhusu umuhimu wa familia ili iweze kuchukua hatua stahiki katika kuimalisha na kuendeleza familia.

Halikadhalika Bi kilangi amewataka washiriki kuitekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya Maadhimisho hayo inayosema “Imarisha Maadili na Upendo kwa Familia imara” hatua ambayo itamsukuma kila mwanafamilia kuwajibika kwa nafasi yake ikiwemo kutenga muda wake wa kukaa na familia ikiwa ni pamoja na kuwapatia malezi mema watoto.

Maadhimisho ya Siku ya kimataifa ya familia mkoani Mtwara yalihudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wananchi wa kawaida, wadau kutoka taasisi za kiraia pamoja na viongozi wa dini ambapo wamejadili na kuweka mikakati kuhusu namna ya kuimarisha malezi bora katika ngazi ya familia kama njia ya kuepukana na wimbi la vitendo vya ukiukwaji wa maadili katika jamii.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC SAWALA AAGIZA VYAMA VYA USHIRIKA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA WAKULIMA.

    June 24, 2025
  • MKURUGENZI MPYA NANYAMBA NA DAS MPYA MTWARA WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

    June 23, 2025
  • MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA UTEGEMEZI KWA WAFADHILI.

    June 28, 2025
  • MAREKANI KUTUMIA BANDARI YA MTWARA KUSAFIRISHA BIDHAA

    June 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.