• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

TPDC YAANZA ZOEZI LA KUKUSANYA TAARIFA ZA UTAFUTAJI WA MAFUTA NA GESI ASILI KITALU CHA MTWARA-LINDI

Posted on: August 5th, 2025

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC ) limeanza kutekeleza zoezi la kuongeza uelewa kuhusu ukusanyaji wa taarifa za mitetemo katika kitalu cha utafutaji wa Mafuta na Gesi Asili cha Lindi na Mtwara.


Zoezi hilo limetambulishwa rasmi kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo Augusti 05,2025 katika kikao kilichohudhuriwa na viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea taarifa ya zoezi hilo litakalochukua miezi 18 na kuhusisha vijiji zaidi ya 30 mkoani humo, Kanali Sawala ameeleza kuwa huo ni muendelezo wa mafanikio makubwa yanayoendelea kupigwa na Serikali katika sekta ya nishati nchini.


Kanali Sawala amesema kuwa utekelezaji wa zoezi hilo utaenda sambamba na fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo upatikanaji wa ajira za muda mfupi zitakazohusisha uchorongaji wa mashimo na ilinzi wa Vifaa.


“Fursa zingine ni za uuzaji wa bidhaa mbalimbali, utoaji wa huduma muhimu ikiwemo chakula na malazi ambavyo vyote vitawawezesha wananchi kupata na kuongeza kipato”


“Zipo pia faida za kiuchumi ambazo ni matazamio ya baadae ambapo upatikanaji wa mafuta na gesi katika eneo hili utawezesha nchi yetu kuwa na uhakika wa nishati ya mafuta au gesi yatakayotumika ndani na nje ya nchi hivyo kuongeza mapato ya Serikali” amesema Kanali Sawala.

Kwa upande wake Meneja msaidizi wa mradi huo Mjiolojia Venance Emmanuel, amesema kuwa zoezi hilo linahusisha uchukuaji wa taarifa za mitetemo kisayansi na litahusisha mikoa ya Mtwara na Lindi.


“Lengo kuu ni kukusanya taarifa sahihi na za kina kuhusu muundo wa kijiolojia chini ya ardhi zikazosaidia kutambua maeneo yenye uwezekano mkubwa wa kuwa na hifadhi kubwa ya mafuta nangesi” ameeleza Venance.


Kuhusu taarifa kwa jamii ameeleza kuwa tayari wameshaanza na wanaendelea kukutana na wananchi katika vijiji vyote vinavyopitiwa na zoezi hilo, na kumekuwa na mwamko mkubwa wa wananchi kujitokeza na kupata taarifa za kina.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MSIMU WA 4 WA MADAKTARI WA SAMIA; MTWARA YAPEWA MADAKTARI BINGWA 54

    September 15, 2025
  • CAG ZIARANI MTWARA; AIPONGEZA OFISI YA MKUU WA MKOA KWA KUPATA HATI SAFI

    September 15, 2025
  • BALOZI WA URUSI AVUTIWA NA UTALII MTWARA

    September 10, 2025
  • “KALAMU YA MWANA HABARI INA NGUVU, ITUMIKE VIZURI” RC SAWALA

    September 10, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.