• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

TUMIENI PEMBEJEO ZA RUZUKU KUONGEZA TIJA SHAMBANI

Posted on: October 23rd, 2023

M/Kiti wa bodi ya mamlaka ya udhibiti wa mbolea Tanzania (TFRA) Dkt Anthony Diallo amewaagiza viongozi na watendaji katika ngazi za Wilaya na Mkoa kusimamia vema pembejeo za ruzuku zinazotolewa na serikali ili ziweze kuongeza tija katika sekta ya kilimo halikadhalika kumkwamua mkulima kiuchumi.


Dkt Diallo ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara ambapo pia aliambatana na baadhi ya wajumbe wa bodi na menejiment ya TFRA na kusisitiza kuwa kila mtu anapaswa kutambua kuwa pembejeo zinazoletwa na serikali zinatokana na kodi ya wananchi hivyo ni vema zikatumika kama ilivyoelekezwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.


“ Mhe Mkuu wa Mkoa sote tunaona ni kwa kiasi gani Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan amejitoa kumsaidia mkulima wa Tanzania, sasa ni jukumu lenu kuhakikisha mnasimamia kikamilifu zoezi zima la kuwasajili wakulima katika kanzi data ili kupata takwimu sahihi za mahitaji yao ya pembejeo” alisema Dkt Diallo.

“Binafsi nawapongeza sana sekretarieti ya Mkoa kwa kazi kubwa ya kusimamia mchakato mzima wa kusambaza mbolea ya ruzuku kwa wakulima lakini pamoja na jitihada hizo pia msiyasahau maeneo mengine ikiwemo eneo la udhibiti wa rasilimali za kilimo, tuna taarifa baadhi ya maafisa kilimo wanakiuka matumizi ya pikipiki walizopewa na serikali, inasemekana wengine wanazifanya bodaboda na wengine wanabebea magendo, naomba muwe wakali katika hili” alisisitiza Dkt Diallo.

Pia Dkt Diallo amewaagiza wakuu wa Wilaya ambao ni wenyeviti wa kamati za pembejeo katika maeneo yao kukaa vikao vya mara kwa mara na wakulima na wamiliki  wa maduka ya pembejeo ili kupata taarifa za mahitaji na changamoto zao hatua ambayo amesema itapunguza wimbi la migogoro wakati wa zoezi la ugawaji wa pembejeo.

Akijibu hoja za wamiliki wa maduka ya kusambaza pembejeo za ruzuku ikiwemo suala la utofauti wa bei kati ya eneo moja na jingine, tatizo la mtandao pamoja na ukosefu wa takwimu sahihi za wakulima Dkt Diallo amewaagiza viongozi na wataalamu katika ngazi zote kufanya vikao vya mara kwa mara na wamiliki hao hatua ambayo amesema itafungua mlango wa kuzipatia suluhisho changamoto zao.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abba Ahmed amemhakikishia M/Kiti huyo wa bodi kuwa wataalamu kutoka Sekretarieti ya Mkoa watafanya kila liwezekanalo kutatua changamoto zilizojitokeza kwa kushirikiana na wataalamu wa kilimo katika ngazi zote ili kuhakikisha jitihada za Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan za kumkomboa mkulima na kuongeza tija katika sekta ya kilimo zinapata mafanikio.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.