• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

TUNATEKELEZA ILANI KWA VITENDO - DANIEL CHONGOLO_KATIBU MKUU CHAMA CHA MAPINGUZI.

Posted on: July 16th, 2023

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi  (CCM)  Mhe Daniel Chongolo amesema kazi kubwa ya chama kwa sasa ni kutimiza malengo iliyojiwekea katika ilani yake ikiwemo kutekeleza ahadi zilizotolewa katika kampeni za uchaguzi mkuu uliopita ikiwemo kutatua kero za Wananchi.



Mhe Chongolo ametoa kauli hiyo katika mkutano wa hadhara kwa mikoa ya Kanda ya kusini uliofanyika katika uwanja wa CCM Nangwanda Sijaona na kusisitiza kuwa miradi ya maendeleo inayogharimu mabilioni ya fedha inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ya ukanda huo ni kielelezo cha utekelezaji wa ilani ya CCM kwa Vitendo.


Aidha Mhe Chongolo amewaeleza maelfu ya wafuasi wa Chama hicho na wakazi wa mji wa Mtwara kuwa CCM haitachoka kuwatumikia na kuwatetea kama ilivyoahidi katika ilani yake huku akitolea Mfano suala la Bandari ambalo amesema limewekwa wazi huku akiwataka Kuwa makini na wapotoshaji wenye nia ovu na Maendeleo ya Watanzania.


Aidha kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi kwa kipindi Cha miaka miwili iliyopita imeweka historia Mkoani Mtwara Kwa kuwekeza kiasi Cha shilingi bilioni 619.6 kutekeleza miradi ya kimkakati.

Kanali Abbas ametoa Kauli hiyo wakati akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Taifa Mhe Daniel Chongolo katika Mkutano wa hadhara katika uwanja wa CCM Nangwanda mjini Mtwara na kusema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo katika sekta za Afya, Elimu, Maji, barabara na umeme umeongeza tija katika shughuli za maendeleo na hivyo kuwapunguzia kero Wananchi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.