• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

TUONGEZE JITIHADA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA: KANALI AHMED ABBAS AHMED

Posted on: March 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed abbas Ahmed amesema kuwa lengo kuu la kuadhimisha siku ya wanawake duniani ni kukumbusha wajibu wa kila mmoja katika jamii  kupigania haki za wanawake hasa katika kutokomeza unyanyasaji unaofanywa na makundi mengine dhidi yao kwani mchango wao ni mkubwa hasa katika ukuaji wa maendeleo.


Kanali Abbas ameyasema hayo katika sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani kimkoa, yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Amani, katika Wilaya ya Tandahimba na kusisitiza kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wa wanawake katika ukuaji wa jamii na uchumi.

“Ni jukumu letu sote kutambua  na kuhakikisha kuwa  wanawake na wanaume wanaongeza mshikamano na kudumisha usawa ndani ya familia ambako ndiko chimbuko la mambo yote kwani mambo haya yakianzia katika ngazi ya familia itakuwa rahisi jamii kuwa na mtazamo wa pamoja kutambua nafasi ya mawanamke katika usawa” alisema Kanali Abbas. 


Aidha kanali Abbas amewataka wananchi wote kuadhimisha siku ya wanawake kwa kutathimini na kutafakari kwa pamoja  njisi gani Mkoa umepiga hatua katika  kutokomeza changamoto zinawakabili wanawake katika jamii na kuongeza jitihada pale ambapo hawajafanikiwa jambo ambalo litaleta usawa wa kijinsia ambao ni chahu ya maendeleo katika jamii.


Pia amewapongeza wanawake wa Mtwara kwa kujitoa kwao na  kuweka mikakati mizuri yenye malengo  ya kukuza Mkoa kiuchumi, kijamii, kidiplomasia na kisiasa, na kusema kuwa anaamini kwa ushirikiano waliouonyesha unaenda kuifanya kazi ya kuufungua Mkoa wa Mtwara kuwa rahisi na kuwataka waandae takwimu itakayowaonesha tathimini ya maendeleo yao kila mwaka.


Halikadhalika Kanali Abbas amesema kuwa  licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali kuweka mazingira mazuri kwa watoto wa kike kushiriki kikamilifu katika elimu bado  tatizo la mimba za utotoni limekuwa kikwazo kikubwa jambo linalopelekea kuathiri afya, elimu na haki ya mtoto wa kike na kumfanya kushindwa kujenga  maisha bora ya baadae.


Kanali Abbas amesisitiza kuwa ni jukumu la wananchi wote katika jamii, taasisi zisizo za kiserikali na wadau kwa ujumla kupambana na mimba za utotoni ili kufikia malengo ya kumkomboa mtoto wa kike na kumuwezesha kufikia ndoto zake na Serikali itaendelea kusimamia   utekelezaji wa mkakati, sheria na sera zinazopinga aina zote za ukatilina kutokuzingatia utawala wa sheria na haki za binadamu.


MWISHO.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2022 November 24, 2021
  • Majina ya watumishi wa umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo February 09, 2018
  • KUFANYA MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19 August 30, 2021
  • Matokeo ya Kidato cha NNe 2017 January 30, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • IGENI MFANO WA MTWARA KUBORESHA ELIMU – WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA, PROF ADOLF MKENDA.

    March 16, 2023
  • TUONGEZE JITIHADA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA: KANALI AHMED ABBAS AHMED

    March 08, 2023
  • NIMERIDHISHWA NA UBUNIFU WA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU¬_WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU MHE. PROF JOYCE NDALICHAKO.

    March 06, 2023
  • LETENI MAONI YENU TUTABORESHA MFUMO WA UTOAJI HAKI_JAJI MKUU MSTAAFU OTHMAN CHANDE.

    February 28, 2023
  • Tazama Zote

Video

Wakulima Mtwara wachangamkia kilimo cha Ufuta
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • NBS
  • IKULU
  • UTUMISHI
  • SALARY SLIP
  • e-GA

Kurasa Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.