• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

VIONGOZI WA VYAMA VYA MSINGI WATAKIWA KUTOKUTUMIKA KISIASA

Posted on: June 20th, 2024

Viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) wametakiwa kutotumika kisiasa na badala yake kufanya kazi kwa weledi kwa lengo la kuwasaidia wakulima.

Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala wakati wa Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Mtwara ambapo pia amewataka Viongozi wote wa AMCOS na Vyama Vikuu vya Ushirika MAMCU na TANECU kuwatumikia wanachama ambao ndio wakulima kwa uaminifu,uadilifu pamoja na kuwalipa stahiki zao kwa wakati.

Amevipongeza vyama vya ushirika Mamcu na Tanecu kwa mafanikio makubwa waliyoyapata kwa kuendelea kusimamai mauzo ya mazao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani pamoja na kununua shamba lenye hekari 1500 kwaajili kulima mazao mbalimbali kwa upande wa Mamcu na Tanecu kujenga kiwanda kikubwa cha kubangua korosho na kutoa ajira kwa maafisa ugani ili kuwa karibu na wakulima waweze kupata kero haraka kupitia maafisa ugani hao.

"Niwapongeze sana wana Ushirika kwa kazi nzuri mnayoifanya wote Mamcu na Tanecu,tumeona Mamcu mmenunua shamba hekari zisizo pungua 1500 na mmeshalima hekari 500 mnahitaji pongezi najua mtaweka jitihada ya kulima zaidi kipindi kijacho na nitakuwa nione ufuta mmepata kiasi gani,mbaazi na korosho zitakapoanza kuvunwa"

"Vilevile Tanecu mmejenga ukuta kwenye ghara lenu pale Tandahimba,mmejenga kongani me naita kongani mana hamtaishia tu kujenga kiwanda,lakini pia mnaendelea kurudisha kwa jamii maeneo mbalimbali hii yote ni kurudisha kile ambacho kinapatikana kwa wananchi wetu."Amesema Sawala

Aidha wale wote ambao wamepata elimu juu ya utumiaji wa mfumo mpya wa mauzo ya mazao unaojulikana kama TMX kutoa elimu kwa wanachama na wakulima ili waweze kujua mfumo huo unavyofanya kazi ili kuepusha taharuki.

Na amewataka viongozi kusimamia vizuri ugawaji wa pembejeo na kufanya kazi kwa uaminifu ili kuongeza uazalishaji wa zao la korosho pia amewaagiza bodi ya korosho kutoa taarifa kwa mkuu wa Mkoa juu ya ugawaji wa pembejeo kilasiku.

"Naombeni kwa namna mlivyoahidi kufanya kazi zenu kwa uaminifu nendeni mkafanye kazi hizo kwa weledi mkagawe pembejeo hizo,ni kitu kisichoingia akilini pembejeo zipo ghalani alafu watu hawapei watu wa vyama vikuu viongozi mko hapa pembejeo zipo magharani alafu wakulima hawapewi mimi nitachukulia watu wanasababu binafsi ambazo hatutokubali,Bodi ya korosho na wakuu wa wilaya nitataka nipate taarifa kila siku jioni nipate taarifa ya hali ya ugawaji wa pembejeo kwa wakulima wetu kila eneo."Amesema Sawala

Nae Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Tandahimba na Newala (TANECU) Karim Chipola, amesema kuwa vyama hivyo wamepanga kuongeza uzalishaji wa zao la korosho,mbaazi na ufuta kwa kuanza kuchukua hatua ya kuanzisha mashamba makubwa ya korosho na ufuta na kuboresha huduma za kiugani kwa wakulima.

Pia amesema ushirika kwa pamoja wamejipanga kutatua changamoto ya kukosekana kwa wanunuzi kwenye mnada hivyo  wamejipanga kusafirisha maafisa masoko kwenda nje ya nchi ili kuangalia masoko ya mazao ya ufuta,mbaazi na korosho ili kukabiliana na changamoto za kwenye minada.


Juni 20, 2024.

#TunaifunguaMtwara

#KaziIendelee

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.