• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Wabanguaji wadogo wa ndani kuwezeshwa kupata korosho

Posted on: March 3rd, 2018

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mheshimiwa Charles Mwijage akikagua uzalishaji wa korosho katika Kiwanda cha Kubangua korosho cha CC 2005 kilichoko mjini Mtwara


WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mheshimiwa Charles Mwijage ameahidi kuanza mchakato wa kuwawezesha wabanguaji wa ndani kupata korosho. amesema kwa hali ilivyo sasa wabanguaji hawa wamekuwa na changamoto ya kupata korosho kutokana na taratibu za kisheria tulizojiwekea.

Mheshimiwa Mwijage ameyasema hayo leo wakati akikabidhi kwa mkandarasi SUMA JKT eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha wajasiliamali katika eneo la Viwanda vidogo mkoani Mtwara.

Amesema kuwa wabanguaji wa ndani hawapati korosho ghafi za kutosha kuendeleza viwanda vyao kutokana na ugumu uliopo kisheria ambapo pamoja na mambo mengine wanahitaji kuingia katika ushindani na makampuni makubwa.

Amesema musimu wa 2016/2017 Tanzania ilisafirisha tani 320,000 ambapo hitaji la wabanguaji wadogo wa ndani ni tani 240. Amesema hilo halikubaliki hivyo serikali itahakikisha wanapata malighafi na kuendeleza viwanda vyao.

 “Tunashindwa kuelewa kuwa tunapotengeneza ajira za hawa akina mama zina tija kuliko kupeleka nje ya nchi… unapotengeneza ajira mtu anakuwa na amani… tumeongozwa na sheria kuliko kutumia sheria.” amesema Mhe. Mwijage


 Awali Akitoa taarifa ya shirika hilo Meneja wa shirika la viwanda vidogo vidogo Mkoa wa Mtwara Joel Chidabwa alisema kuwa mkoa wa Mtwara umekuwa na ongezeko kubwa la watu kutokana na ugunduzi wa Gesi asilia  na hivyo kumekuwepo na ongezeko la mahitaji ya bidhaa mbalimbali za kutoka viwandani. Amemtaka Mheshimiwa Waziri kusaidia kuondoa changamoto wanazokutana nazo ili wapate nguvu ya kuwandeleza wajasiliamali hao.

 “Tunazo zaidi ya hekali 6 ambazo ziko wazi hazijaendelezwa na zinaweza kutumiwa kwa ajili ya viwanda kwa kujenga majengo ambayo yanaweza kutumika kwa shughuli mbalimbali za viwanda” alisema Chidabwa

Kwa upande wake Mbunge wa Mtwara Vijijini Hawa Ghasia alisema pamoja na mambo mengine kuna tatizo kubwa la umeme na maji mkoani Mtwara hali ambayo inaathiri wawekezaji wadogo kushindwa kufanyakazi ipasavyo.

“Msisema wajasiliamali ni wavivu wanapoingiza bidhaa zao kila baada ya dakika mbili umeme unakatika bidhiaa zinaharibika  anapata hasara. Haya mambo lazima yawe na uwiano. Unapoweka kiwanda hakikisha umeme na maji yapo na mtetezi wa haya mambo ni Waziri wa Viwanda na Biashara”  amesema Ghasia



Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.