• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WAELIMISHENI WAKULIMA WAONDOKANE NA UTAMADUNI WA KUTEGEMEA ZAO LA KOROSHO PEKEE_KANALI AHMED ABBAS AHMED, MKUU WA MKOA WA MTWARA.

Posted on: February 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewataka wadau wa kilimo kuja na suluhisho litakalomsaidia mkulima kuondokana na utamaduni wa kutegemea zao la korosho kama chanzo  pekee cha mapato kwani wanaweza kuathirika kiuchumi endapo uzalishaji wake utashuka kama ilivyojitokeza katika msimu wa kilimo 2022/2023.

Kanali Abbas ametoa kauli hiyo katika kikao cha tathmini ya kilimo ngazi ya Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa BOT mjini Mtwara, ambapo amesema umefika wakati wataalamu na wadau wote wa kilimo watoe majibu sahihi yatakayotoa dira ya kumkomboa mkulima na kuinusuru sekta ya kilimo kwa ujumla,

“Ndugu wajumbe wa kikao hiki, kila mmoja wetu hapa ni shahidi, uzalishaji wa zao letu mama na la kimkakati la Korosho umeathiriwa na mabadiliko ya tabia ya nchi, halikadhalika mabadiliko ya bei katika soko la dunia” aliwaeleza wajumbe Kanali Ahmed Abbas Ahmed.

“Sasa hatuwezi kukaa tunalalamika tu, binafsi ninaamini kikao hiki leo kitatoa mwelekeo wa namna tutakavyosimamia kwa tija sekta ya kilimo mkoani kwetu ili kumpa matumaini mkulima shambani asione nguvu zake zinapotea bure” aliongeza kanali Abbas.

Pia Mkuu wa Mkoa Kanali Ahmed Abbas Ahmed amekitumia kikao hicho kuwaeleza wajumbe kuwa mkoa umekuwa ukitegemea mazao ya kimkakati kwa muda mrefu ikiwemo korosho na ufuta, mazao ambayo yamekuwa yakichangia sehemu kubwa ya pato la la mkoa na kuongeza kuwa kuathirika kwa soko  na uzalishaji wake hivi karibuni unaulazimu mkoa kukuna kichwa.

“Ndugu wajumbe, nitumie fursa hii kuwaelekeza wataalamu wetu wa kilimo na wadau wote kuwaelimisha wakulima wetu umuhimu wa kulima mazao mchanganyiko ikiwemo ufuta, karanga na mengine, ninaamini kilimo cha aina hiyo kitaongeza tija kwa kuleta matumaini mapya kwa mkulima” alisisitiza Kanali Abbas.

Aidha Kanali Abbas pia amewataka wajumbe na wataalam kutathmini ni kwanini Mkoa umeshindwa kufikia malengo ya kuzalisha tani 240,000 za korosho katika msimu wa kilimo wa 2022/2023 ili kwa pamoja waweze kuja na maazimio yatakayoleta tija msimu ujao.

Akizungumzia mwenendo wa mauzo ya zao la korosho, Kanali Abbas amesema mpaka kufikia mwezi Januari 2023 tayari ilikuwa imefanyika minada 24 katika maeneo mbalimbali ambapo jumla ya tani 94,000 za korosho ghafi zenye thamani ya Shilingi bilioni 176 tayari zilikuwa zimeuzwa katika Vyama Vikuu vya Ushirika vya TANECU na MAMCU.

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa Mkoa wa Mtwara Alli Linjenje amewaeleza wajumbe kuwa pamoja na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na  kushuka kwa bei katika soko la dunia bado ipo changamoto ya wakulima kukataa kuuza korosho zao katika minada.

“Mheshimiwa Mwenyekiti tumekuwa tukipokea taarifa za wakulima kutoridhishwa na bei na hivyo kubaki nazo nyumbani” alisema Bwana Linjenje.

Linjenje alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanaendelea kuwaelemisha wakulima ili kuwaepusha kuingia katika utaratibu usio rasmi wa mauzo ya korosho maarufu kama Kangomba.

Naye  Mkurugenzi wa bodi ya  Korosho Tanzania (CBT) Francis Alfred ametoa takwimu za uzalishaji na mauzo ya korosho ghafi kupitia chama kikuu cha ushirika TANECU kuwa ni tani 33,062,163 sawa na  asilimia 19 zenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 62.

Kwa upande wa chama kikuu cha ushirika cha MAMCU, Bwana Alfred amesema kimeweza kununua tani 59,609,667 za korosho ghafi sawa na asilimia 34 zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 111.

Kikao hicho cha siku moja kiliwakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wataalamu wa kilimo kutoka halmashauri za wilaya, Viongozi wa Wilaya na Mkoa, Wenyeviti wa halmashauri, wadau kutoka Vyama Vikuu vya Ushirika pamoja na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.