• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

Wafanya biashara na Wajasiliamali Changamkieni Fursa Commoro;Serikali ya Mkoa Itawaunga Mkono_Kanali Ahmed Abbas Ahmed, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

Posted on: December 14th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewahaidi wafanyabiashara na wawekezaji wanaodhamiria kuwekeza upande wa Tanzania hususani katika mkoa wa Mtwara, kuwa serikali ya mkoa tayari imeunda kamati ambayo imepewa jukumu la kubaini changamoto zinazokwamisha biashara kati ya pande hizo mbili ili ziweze kutatuliwa kwa haraka.


Kanali Abbas ametoa kauli hiyo mjini Moron, katika uzinduzi wa maonesho ya kimataifa ya biashara yanayoshirikisha wafanyabiashara kutoka nchi mbalimbali, wengi wao wakitoka Mkoa wa Mtwara Tanzania, ambao kijiografia ndio uko jirani na nchi ya Commoro.


Akizungumza na wafanyabiashara walioshiriki katika katika maonesho hayo katika viwanja vya ubalozi wa Tanzania mjini Moron nchini Commoro, Mhe Abbas amesema kuwa Serikali ya Tanzania kupitia uongozi wa mkoa wa Mtwara tayari umebaini baadhi ya changamoto zinazowakabili wafanyabiashara kati ya Commoro na ukanda wa pwani ya kusini hususani mkoa wa Mtwara Tanzania na tayari wameanza kuzifanyia kazi.

"Ndugu zangu mliohudhuria maonesho haya, naomba nichukue fursa hii kuwahakikishia kuwa Tanzania na Commoro mbali na biashara, tuna historia ya muda mrefu, sisi ni ndugu; Kwahiyo uhusiano wetu kibiashara pia unalenga kuimarisha mahusiano yetu kidiplomasia na kiuchumi" aliongeza Kanali Ahmed Abbas Ahmed.


Aidha Kanali Abbas amesisitiza kuwa kufuatia kamati iliyoundwa na uongozi wa Mkoa wa Mtwara ambao ni mbia mkubwa wa biashara na nchi ya Commoro ilitoa mapendekezo ya kupata meli kubwa itakayopunguza  adha ya usafirishaji wa bidhaa za wafanyabiashara kati ya Tanzania na Commoro.

"Naomba nichukue fursa hii kuwahakikishia wafanyabishara kutoka pande zote mbili, kuwa kamati yetu tayari imekuja na mwarobaini wa kurahisisha usafirishaji wa bidhaa zenu kutoka Tanzania kuja Commoro, hivyo naomba mvute subira kidogo mpango huu utakamilika hivi karibuni" alisisitiza Kanali Ahmed Abbas.


Katika maonyesho hayo ambayo pia yalihudhuriwa na balozi wa Tanzania nchini Commoro Mhe. Perreira Silima, Kanali Abbas  anatarajia kuongoza mkutano utakaowakutanisha wafanyabiashara kutoka Tanzania na Commoro pamoja na uongozi wa Chemba ya biashara ya nchi hiyo.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.