• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WANAMTWARA TUSHIKAMANE KATIKA SHIDA, RAHA HALIKADHALIKA WAKATI WA KUTEKELEZA SHUGHULI ZA MAENDELEO - KANALI AHMED ABBAS AHMED

Posted on: February 27th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed, leo ameungana na mamia ya waombelezaji katika msiba wa mfanyabiashara wa siku nyingi katika  soko kuu la Mtwara Marehemu Fakhi Nyambi Luyeye aliyefariki dunia juzi katika hospitali ya Ligula baada ya kuugua kwa muda mrefu.


Akiambatana na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama Kanali Abbas alifika nyumbani kwa marehemu eneo la Sabasaba leo, majira ya mchana na kusema kuwa anafarijika kuwaona wanamtwara wanashirikiana kwa hali na mali katika shida na raha.

“Ndugu waombolezaji, naomba nichukue fursa hii kuwapeni pole kwa msiba huu mzito wa mpendwa wetu, ninaomba mwenyezi Mungu awape subira na hekima hasa katika kipindi hiki kigumu ambacho hakizoeleki kwa binadamu” aliwaeleza waombolezaji Kanali Abbas.


Pia Kanali Ahmed Abbas Ahmed alitumia jukwaa la msiba huo kuwaeleza waombolezaji kuwa mshikamano walionao usiishie wakati wa matatizo pekee bali waendelee kuutekeleza kwa vitendo ikiwemo kushirikiana na Serikali kutatua changamoto zinazoikabili jamii.

“Ndugu wafiwa na waombolezaji nisingependa kuchukua muda wenu mrefu, lakini naomba mniruhusu niwaeleze kwa ufupi machache kuhusu Mkoa wenu” aliongeza Kanali Abbas.


Kanali Abbas aliwakumbusha waombolezaji kuwa Mkoa wa Mtwara umepata heshima kubwa ya kuzindua mwenge wa uhuru Aprili 2 mwaka huu na kuwataka kushiriki kikamilifu katika hatua zote za maandalizi.

Halikadhalika Kanali Abbas ameitumia fursa hiyo kuuarifu umma wa wanamtwara kuhusu ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mkoani Mtwara inayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii.

“Mhe Waziri Mkuu ametupa heshima ya kuutembelea mkoa wetu, tunatarajia atatembelea Wilaya na Halmashauri zetu zote, hivyo nawaomba mjitokeze kwa wingi kumlaki popote atakapopita, lakini pia kama kuna jambo au tatizo lolote linalowasibu na mnadhani nina uwezo wa kulitatua niambieni sasa kuliko kumsubiri mgeni” alisisitiza kanali Ahmed Abbas Ahmed.


Akizungumza kwa niaba ya familia ya wafiwa Alhaji Dadi Mbulu amemshukuru Mkuu wa Mkoa na kamati yake ya Ulinzi na Usalama kwa kuonyesha ukaribu na wananchi na kusema kuwa kitendo hicho ni ishara njema ya viongozi wanaojali watu.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Hanafi Msabaha amewahakikishia mamia ya waombolezaji kuwa yuko tayari kushirikiana na Wanamtwara wakati wowote atakapohitajika huku akiwaomba kumpa ushirikiano katika matukio yote ya kitaifa ikiwemo Uzinduzi wa Mwenge na Ziara za viongozi wakuu.


MWISHO.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2022 November 24, 2021
  • Majina ya watumishi wa umma wanaostahili kulipwa madai ya malimbikizo February 09, 2018
  • KUFANYA MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19 August 30, 2021
  • Matokeo ya Kidato cha NNe 2017 January 30, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • IGENI MFANO WA MTWARA KUBORESHA ELIMU – WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA, PROF ADOLF MKENDA.

    March 16, 2023
  • TUONGEZE JITIHADA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA: KANALI AHMED ABBAS AHMED

    March 08, 2023
  • NIMERIDHISHWA NA UBUNIFU WA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU¬_WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU MHE. PROF JOYCE NDALICHAKO.

    March 06, 2023
  • LETENI MAONI YENU TUTABORESHA MFUMO WA UTOAJI HAKI_JAJI MKUU MSTAAFU OTHMAN CHANDE.

    February 28, 2023
  • Tazama Zote

Video

Wakulima Mtwara wachangamkia kilimo cha Ufuta
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • NBS
  • IKULU
  • UTUMISHI
  • SALARY SLIP
  • e-GA

Kurasa Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.