• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WAZIRI JAFO AVUTIWA NA MJASIRIAMALI ANAETENGENEZA MASHINE ZA KUBANGUA KOROSHO, AAGIZA SIDO KUMUWEZESHA.

Posted on: August 8th, 2025

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameliagiza Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO )kumtembelea na kumuwezesha maarifa zaidi mjasiriamali, Ndg. Abdul Saidi Kichupa anaetengeneza mashine za kubangua korosho, kila moja ikiwa na uwezo uwezo wa kubangua kilo 150 kwa siku.


Waziri Jafo ametoa agizo hilo mapema leo tarehe 08 Agosti 2025 kwenye kilele cha maadhimisho ya Nanenane kanda ya kusini alipotembelea banda la Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba ambapo alielezwa kwa sasa mjasiriamali huyo ameshatengeneza mashine saba.

“Naomba nikutanishwe na huyu mjasiriamali, nimependa anachokifanya. Pia nawaagiza SIDO kumtembelea kumuwezesha, tukiwa na mashine nyingi za wajasiriamali wadogo zenye kubangua kilo 150 kwa siku tutapiga hatua kubwa katika sekta ya viwanda pia tutaliongezea zao la korosho thamani. Lakini pia nitoe rai apewe kipaumbele kwenye mikopo.” Alieleza Mhe. Jafo


Ndg. Kichupa ni miongoni mwa vijana waliopata ujuzi wa kutengeneza mashine za kubangua korosho kutoka kwa kijana mbunifu, Ndg. Zaidu Mbwana.


Waziri Jafo amezipongeza Halmashauri za Mikoa ya Mtwara na Lindi kwa kutoa mikopo ya 10% kwa wajasiriamali kwa kuzingatia 4% wanawake, 4% vijana na 2% walemavu huku akitoa rai kwa wananchi kupenda kununua vitu vinavyozalishwa na wajasiriamali wazawa ili kukuza uchumi wa nchi.

Akizungumza mbele ya Waziri Jafo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha kilimo cha mazao ya chakula ili fedha zinazopatikana baada ya kuuza mazao ya biashara zitumike kwa shughuli za maendeleo.


Maonesho ya Nanenane yameambatana na utoaji zawadi kwa washiriki waliofanya vizuri kisekta ambapo Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba imeibuka kidedea kati ya Halmashauri 15 za mikoa ya Mtwara na Lindi zilizofanya vizuri zaidi. Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba pia imeng’ara katika washiriki wa jumla ambapo imeshika nafasi ya tatu.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MSIMU WA 4 WA MADAKTARI WA SAMIA; MTWARA YAPEWA MADAKTARI BINGWA 54

    September 15, 2025
  • CAG ZIARANI MTWARA; AIPONGEZA OFISI YA MKUU WA MKOA KWA KUPATA HATI SAFI

    September 15, 2025
  • BALOZI WA URUSI AVUTIWA NA UTALII MTWARA

    September 10, 2025
  • “KALAMU YA MWANA HABARI INA NGUVU, ITUMIKE VIZURI” RC SAWALA

    September 10, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.