• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WAZIRI KASEKENYA AKAGUA BARABARA YA KIUCHUMI MNIVATA-MASASI, AAHIDI WANANCHI KULIPWA FIDIA AWAMU YA PILI MILIONI 428

Posted on: September 13th, 2024

Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Mhandisi Godfrey Msongwe Kasekenya tarehe jana 13/08/2024 amefanya ziara mkoani Mtwara kukagua miradi ya ujenzi ikiwemo Barabara ya Mnivata-Masasi km 160 ambayo ni sehemu ya Barabara ya kusini itokayo Mtwara hadi Masasi kupitia Wilaya za Mtwara, Tandahimba, Newala na Masasi. 

Barabara hii maarufu kama Barabara ya Uchumi kwani hupita katika maeneo yanayolima kwa wingi zao la Korosho katika Mkoa wa Mtwara inatarajiwa kukamilika tarehe 30/04/2026.

“Lengo la serikali si kujenga barabara halafu iache watu wameumia. Naomba wananchi wafahamu kuwa serikali itatoa fidia kwa wale watakaopitiwa na mradi huu na tayari tathmini ilishafanyika na watu wakalipwa kwa awamu ya kwanza; awamu ya pili tunadaiwa takribani Shilingi Milioni 428 na tayari tumewasilisha maombi Hazina ili pesa ziweze kulipwa.” Alieleza Waziri Kasekenya

Aidha Mhe. Kasekenya aliwataka wakandarasi na pamoja na Mhandisi mshauri kuhakikisha wanatengeza barabara za pembeni ili ziweze kupitika kipindi chote cha ujenzi kwani barabara hiyo ni ya kiuchumi na inaunganisha Halmashauri zote za Mkoa wa Mtwara huku akisisitiza mradi kukamilika kwa wakati na kwa ubora.

Katika hatua nyingine Mhe. Kasekenya alitembelea eneo la Kilambo ambalo ni mpaka wa nchi ya Tanzania na Msumbiji ambapo serikali inatarajia kujenga daraja ili kuunganisha nchi hizo zinazotenganishwa na mto Ruvuma ili kufungua fursa zaidi kiuchumi.

Bw. Dhulkifu Hamdan, Kaimu Meneja wa TEMESA Mtwara (Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania) alimweleza Naibu Waziri wa Ujenzi kuwa kivuko cha Mv Kilambo tayari kimemalizika matengenezo kwa sasa wanafanya utaratibu wa kukirejesha mahali hapo.


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KARIBU MTWARA

    May 17, 2025
  • JESHI LA POLISI TANZANIA YATUPIA JICHO MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA

    May 20, 2025
  • MWENGE WA UHURU MASASI

    May 18, 2025
  • NANYUMBU WAANZISHA BIO ZA MWENGE MTWARA

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.