• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

WAZIRI MBARAWA AELEZA MATUMIZI YA BANDARI YA KISIWA MGAO-MTWARA

Posted on: December 19th, 2024

Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa leo tarehe 19 Novemba 2024 amefanya ziara mkoani Mtwara ambapo ametembelea bandari ya Mtwara na eneo la Kisiwa Mgao itakapojengwa bandari ya kusafirishia mizigo yenye uchafu.

Waziri Mbarawa ameeleza jinsi serikali inavyowekeza kwenye usimamizi wa bandari hususan miundombinu na vitendea kazi. “Mwaka mmoja uliopita bandari ya Mtwara ulikuwa unakuta meli moja kwa siku lakini leo hii nimesimama hapa kuna meli mbili zinapakia zao la korosho. Meli hii inapakia takribani tani 9,000 na meli ile inapakia takribani tani 30,000. Tarehe 21 itakuja meli ya kuleta kifaa kingine ili kuleta ufanisi zaidi wa bandari”

Aidha, Mhe. Mbarawa ametoa rai kwa wafanyakazi kwa bandari kuongeza ufanisi ili meli zikifika bandarini hapo zihudumiwe ndani ya muda mfupi.

Akieleza kuhusu vumbi linalozalishwa ndani ya bandari kutokana na usafirishwaji wa makaa ya mawe, Mhe. Mbawara ameeleza mpango wa serikali wa muda mrefu ambapo itahamisha shughuli zote za usafirishaji na upakuaji wa bidhaa chafu yaani “dust cargo” ikiwemo saruji, mbolea na makaa ya mawe kwenda Kisiwa Mgao ambayo itaanza kujengwa tarehe 03 Januari 2025 na inatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2027 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 434.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala ametumia fursa hiyo kumuomba Waziri huyo wa Uchukuzi kuzungumza na Waziri wa Kilimo ili mbaazi na ufuta inayolimwa ukanda wa kusini isafirishiwe bandari ya Mtwara.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Sawala amemuomba Waziri wa Uchukuzi kurejesha safari za shirika la ndege AirTanzania mkoani Mtwara. Nae, Mhe. Mbawara amelipokea ombi hilo na kuahidi miongoni mwa ndege mpya zitakazonunuliwa zitafanyanya safari mkoani hapa.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • CRDB KANDA YA KUSINI YAISHIKA MKONO MTWARA MAANDALIZI YA UMISETA TAIFA

    May 27, 2025
  • KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, MIKOKO 6,000 YAPANDWA MTWARA.

    May 31, 2025
  • KAMATI YA LISHE MKOA WA MTWARA YAKUTANA

    May 30, 2025
  • MIRADI YA UJENZI ITOE AJIRA KWA WANANCHI” WAZIRI ULEGA

    May 27, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.