Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa amepiga marufuku kuuza mahindi ya kuchoma na kuwataka wananchi kuhifadhi chakula ikiwa ni hatua mojawapo ya kupambana na athari za ugonjwa wa COVID-19
Februali 2019 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara aliagiza wakuu wa wilaya wote mkoani Mtwara kuhamasisha kilimo cha ufuta katika maeneo yao ili kuondokana na kutegemea zao la korosho pekee.
Agizo hilo lilienda sambamba na kuzitaka halmashauri kuanzisha mashamba darasa ya ufuta ambayo yaliwekwa chini ya usimamzi wa wataalamu wa Taasisi ya Utafitiwa Kilimo Tanzania Kituo cha Naliendele (TARI-Naliendele)
Halmashauri ziliitikia wito huo kwa kuanzisha mashamba hayo ambayo sasa yanendelea vizuri.
Pia walisimamia wananchi kuanzisha mashamba ya mtu mmoja mmoja, mashamba ya familia na mashamba ya vikundi vya vijana. Baadhi ya mbinu zilizotumika ni pamoja na kuwagawia wakulima mbegu kwa matarajio ya kuwa baada ya kuvuma watarudisha kiasi kilekile walichopewa ili serikali ya eneo husika ikigawe kwa wakulima wengine.
Wakulima walioitikia wito huo wanaanza kuiona dunia inayowezekana kupitia kilimo cha ufuta. Bwala Udede ni mmoja wa wakulima ambaye anataraji kupata zaidi ya milioni kumi ndani miezi miwili ijayo. Msikilize hapo kwenye video hiyo ya dakika mbili tu.
Jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama Vimeimarisha ulinzi katika mipaka ya Tanzania ili kuhakikisha wahalifu wanaofanya mauaji na vurugu nchini Msumbiji hawapati nafasi ya kuingia Tanzania.
Hayo yamesemwa leo na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Liberatus Sabas wakati akikagua kikosi maalumu cha kupambana na uhalifu nchini kilichowasili mkoani Mtwara kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji.
Amesema wahalifu hao wamekuwa wakivamia kambi za jeshi, vituo vya polisi, kuchoma moto na kuchukua silaha nchini Msumbiji na pia wameripotiwa kuvamia benki na kupora fedha huko huko Msumbiji.
“Kule hali si shwali kama ambavyo mmekuwa mkisikia kwenye vyombo mbalimbali vya habari. Sisi kwa kutambua hilo, na kutambua umuhimu wa sisi kama Taifa, na umuhimu wa wananchi wa Tanzania kuwa shwali tumejipanga kuhakikisha tatizo hili haliji huku kwetu.”
Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwasilisha taarifa za mtu yeyote ambaye wanamtilia shaka.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara
Anuani ya Posta: 544, MTWARA
Simu: +255 23 2333014
Mobile: +255 23 2333014
Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz
Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.